

Lugha Nyingine
新华社评大数据“杀熟”:运用新技术不能坏了老规矩大数据新技术老规矩
Kuanzia Jumamosi, Machi 24 maua ya rapa katika mji wa Guangcang, Wilaya ya Tongzi, Mkoa wa Guizhou nchini China, yalifikia mchanuo wao kamili. Shamba kubwa la rapa lenye ukubwa wa ekari elfu moja limegeuka kuwa bahari ya rangi ya dhahabu yenye uzuri wa aina yake, likivutia watalii kujichangamanisha katika uzuri wa msimu wa mchipuko.
Katika miaka ya hivi karibuni, Wilaya hiyo ya Tongzi imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika uendelezaji utalii wa vijijini. Imechochea kwa kina rasilimali zake za utalii wa vijijini na kuandaa kwa umakini matukio mbalimbali kama vile "Tamasha la Kijiji". Hili limehimiza kwa ufanisi mfungamano wa kina wa utamaduni na utalii, ukitoa msukumo wa kila mara kwa ustawishaji wa vijiji.
Mwaka 2024, Tongzi ilipokea jumla ya watalii zaidi ya milioni 16.89, ikifikia mapato jumuishi ya utalii ya Yuan bilioni 19.39.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma